Jipatie gari nchini Tanzania
Jipatie gari la kuendesha kupitia mpango ambao Uber imeingia ubia na makampuni kutoka jijini Dar es Salaam yatakayokusaidia upate gari.
Je, ni gari gani linafaa zaidi? Hakikisha linatimiza vigezo vya kutumika nchini Tanzania na ukumbuke kwamba utapata pesa nyingi zaidi iwapo ulaji wake wa mafuta ni mdogo.
Benki ya CRDB
Kampuni ya Uber imeingia ubia na Benki ya CRDB ili kukupatia mkopo wa gari mahsusi kwa ajili ya madereva-washirika wanaotumia mfumo wetu.
Maelezo
- Riba: 21- 23%
- Malipo ya awali: kuanzia 0%
- Muda wa marejesho: miezi 12-36
- Thamani ya gari < TZS 14,000,000
Benki ya CRDB inatambua haja ya uwazi pamoja na hatari anazokabiliana nazo mjarisiamali katika kutimiza ndoto zake.
Hii ndio sababu dhamira ya benki ya CRDB ni kuwajengea uwezo wajasiriamali kupitia huduma za kifedha zinazoleta mageuzi makubwa kwa kutosheleza mahitaji ya wajasiriamali na kukuza biashara yao kwa kuleta ufanisi mkubwa na kutoa huduma tofauti tofauti.
Riba zetu zinaanzia 21% kwa mwaka na tunalipia 100% ya gari utakalochukua kwa mkopo ambao utrejesha ndani ya muda wa miezi 12, dhamira yetu ni kutoa mkopo ambao una masharti nafuu ili uikuze biashara yako.
Je, mnaangalia vigezo gani?
- Uwe na tathmini isiyopungua nyota 4.55
- Wastani wa Mapato Ghafi ya nauli yawe TZS 375,000 ndani ya wiki 12 zilizopita
- Uwe umetumia Uber kuendesha gari kwa kipindi kisichopungua miezi 6
Tanzania
Je, una swali lolote? Utajibiwa. Utahudumiwa kwa namna pekee katika Kituo cha Madereva wa Uber katika ofisi za Dar es Salaam.
Anza kutengeneza pesa kwa kuendesha gari ukitumia Uber ukiwa Tanzania
Taarifa inayopatikana kwenye tovuti hii ni kwa madhumuni ya kuhabarisha pekee na huenda isitumike katika nchi, kanda, au jiji lako. Inaweza kufanyiwa mapitio na kubadilishwa bila taarifa yoyote. Uber haina dhamana yoyote kwa bidhaa au huduma zinazotolewa na washirika wetu.